Image captionMbappe aliibuka mchezaji bora chipukizi kwenye michuano ya kombe la dunia na kuisaidia Ufaransa kutwaa taji hilo
Mchezaji kinda Mfaransa Kylian Mbappe na Mwingereza Harry Kane ni miongoni mwa wachezaji walioorodheshwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2018.
Eden Hazard wa Chelsea, Mohamed Salah kutoka Liverpool, Kevin De Bruyne wa Manchester City na mshambuliaji mpya wa Juventus Cristiano Ronaldo https://king360live.blogspot.com/Michezoni miongoni mwa waliojumuishwa.
Lucy Bronze kutoka Uingereza pia amejumuishwa katika tuzo hiyo kwa upande wa wanawake.
Mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane mwenye miaka 24 alishinda kiatu cha dhahabu baada ya kuibuka mfungaji bora katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi akiwa na magoli 6 na kuifanya England kumaliza nafasi nzuri zaidi katika mashindano haya tokea mwaka 1990.
Image captionHazard aliisaidia Chelsea kuibuka mabingwa wa kombe la FA msimu uliopita
Alishiriki michuano hii ya kombe la dunia akiwa tiyari na magoli 30
Aliweza pia kuwa na kiwango kizuri katika michuano ya kombe la dunkwenye ligi kuu England.ia, akiwa mchezaji wa kwanza kutoka England kushinda kiatu cha dhahabu tokea alivyofanya Gary Lineker mwaka 1986.
Hazard mwenye miaka 27 alishinda kikombe cha FA akiwa na Chelsea mwezi Mei na pia kuifikisha timu ya Ubelgiji katika nafasi ya tatu kwenye michuano ya kombe la dunia ikiwa ndio nafasi nzuri zaidi kwa Ubelgiji kuifikia tokea kuanza kwa mashindano haya.
Image captionRonaldo ameshinda mara tatu mfululizo kombe la klabu bingwa Ulaya akiwa na Real Madrid
Salah mwenye miaka 26 alikua pia na msimu mzuri ndani ya Liverpool. Raia huyu wa Misri alifunga magoli 46 kwa upande wa klabu na kwenye timu ya taifa, huku pia akiifikisha Liverpool katika fainali ya klabu bingwa barani Ulaya.
Image captionSalah alikua mchezaji bora wa msimu EPL na pia mfungaji bora akiifikisha Liverpool fainali ya kombe la klabu bingwa Ulaya
Walioorodheshwa
Cristiano Ronaldo - Juventus & Ureno
Kevin De Bruyne - Manchester City & Ubelgiji
Antoine Griezmann - Atletico Madrid & Ufaransa
Eden Hazard - Chelsea & Ubelgiji
Harry Kane - Tottenham & England
Kylian Mbappe - Paris St-Germain & Ufaransa
Lionel Messi - Barcelona & Argentina
Luka Modric - Real Madrid & Croatia
Mohamed Salah - Liverpool & Misri
Raphael Varane - Real Madrid & Ufaransa
Kwa upande wake De Bruyne mwenye miaka 27 alikua na mchango mkubwa sana katika rekodi nzuri iliyowekwa na klabu yake ya Manchester City kwa kufikisha alama 100 na kuipa ubingwa wa EPL. Alifanya vyema pia akiwa na timu yake ya taifa ya Ubelgiji iliyoibuka mshindi wa tatu kwenye kombe la dunia 2018.
Ulikuwa mwaka mzuri pia kwa mshindi mara tano wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo. Mreno huyu alifunga magoli 54 katika michezo 54 ya michuano yote, akiipa pia klabu yake za zamani Real Madrid kombe la klabu bingwa barani Ulaya kwa mara ya tatu mfululizo.
Mwisho wa kupiga kura utakua Agosti 10 na tuzo zitatolewa mjini London Septemba 20.
Image captionLucy Bronze aliisaidia Lyon kupata vikombe viwili msimu uliopita
Kwa upande wa wanawake Lucy Bronze wa England ameorodheshwa baada ya kuwa na msimu mzuri akicheza kama mlinzi wa kushoto.
Bronze mwenye miaka 26 anayechezea Ligi kuu ya Ufaransa ameisaidia Lyon kushinda kikombe cha ligi kuu na kile cha ligi ya mabingwa Ulaya katika msimu wake wa kwanza akiwa na Lyon baada ya kuondoka Manchester City mwezi Agosti.
Walioorodheshwa
Lucy Bronze - Lyon & England
Pernille Harder - Wolfsburg & Denmark
Ada Hegerberg - Lyon & Norway
Amandine Henry - Lyon & Ufaransa
Samantha Kerr - Perth Glory/Chicago Red Stars & Australia
Kiungo wa kimataifa wa Croatia Madrid Luka Modric,ametangazwa kuwa mchezaji bora wa Fifa wa kiume katika shughuli ya utoaji tuzo iliyofanyika usiku huu London Uingereza.
Modric mwenye miaka 33, amewapiga kumbo mchezaji mwenzake wa zamani wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, anayechezea Juventus, kwa sasa pamoja na winga wa Liverpool Mohamed Salah.
Haki miliki ya pichaKING360 MEDIAImage captionMarta Vieira da Silva, ametwaa tuzo ya mchezaji bora kwa mara sita
Kwa upande wa wanawake mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya Orlando Pride, Marta Vieira a Silva, ndie aliyechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Fifa na kuwa ni tuzo yake wa sita ya uchezaji bora akiwazidi Dzsenifer Marozsan na Ada Hegerberg.
Kocha wa mabingwa wa kandanda duniani Ufarasansa Didier Deschamps ameibuka kidedea kuwa ndie kocha bora na kuwapiku Zinedine Zidane na kocha wa timu ya taifa ya Croatia Zlatko Dalic
Haki miliki ya pichaKING360 MEDIAImage captionDidier Deschamps ametwaa tuzo ya kocha bora
Mohamed Salah ametwa tuzo ya goli bora(Puskas) goli ambalo alilifungwa dhidi ya Everton mwezi Desemba.Kipa wa zamani wa Chelsea Thibaut Courtois ametajwa kuwa ndie kipa bora .
Pia katika tuzo hizo kulitangazwa kikosi cha wachezaji kumi na moja wa dunia wa Fifa
Haki miliki ya pichaKING360 MEDIAImage captionKikosi cha nyota kumi na moja wa kikosi cha dunia