Tuesday, September 25, 2018

Luka Modric ateuliwa mchezaji bora wa kiume Fifa, Deschamps kocha bora

https://king360live.blogspot.com/
Kiungo wa kimataifa wa Croatia Madrid Luka Modric,ametangazwa kuwa mchezaji bora wa Fifa wa kiume katika shughuli ya utoaji tuzo iliyofanyika usiku huu London Uingereza.
Modric mwenye miaka 33, amewapiga kumbo mchezaji mwenzake wa zamani wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, anayechezea Juventus, kwa sasa pamoja na winga wa Liverpool Mohamed Salah.



Marta Vieira da Silva, ametwaa tuzo ya mchezaji bora kwa mara sitaHaki miliki ya pichaKING360 MEDIA
Image captionMarta Vieira da Silva, ametwaa tuzo ya mchezaji bora kwa mara sita

Kwa upande wa wanawake mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya Orlando Pride, Marta Vieira a Silva, ndie aliyechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Fifa na kuwa ni tuzo yake wa sita ya uchezaji bora akiwazidi Dzsenifer Marozsan na Ada Hegerberg.
Kocha wa mabingwa wa kandanda duniani Ufarasansa Didier Deschamps ameibuka kidedea kuwa ndie kocha bora na kuwapiku Zinedine Zidane na kocha wa timu ya taifa ya Croatia Zlatko Dalic



Didier Deschamps ametwaa tuzo ya kocha boraHaki miliki ya pichaKING360 MEDIA
Image captionDidier Deschamps ametwaa tuzo ya kocha bora

Mohamed Salah ametwa tuzo ya goli bora(Puskas) goli ambalo alilifungwa dhidi ya Everton mwezi Desemba.Kipa wa zamani wa Chelsea Thibaut Courtois ametajwa kuwa ndie kipa bora .
Pia katika tuzo hizo kulitangazwa kikosi cha wachezaji kumi na moja wa dunia wa Fifa



Nyota kumi na moja wa kikosi cha duniaHaki miliki ya pichaKING360 MEDIA
Image captionKikosi cha nyota kumi na moja wa kikosi cha dunia

1 comment: